Maafisa wa afya wa Umoja wa Mataifa wanasema kumetokea maambukizi mapya ya Ebola nchini Liberia chini ya miezi mitatu baada ya nchi hiyo kutangazwa kutokuwa na ugonjwa huo.
Wachambuzi wanasema habari hii ni pigo kubwa kwa nchi ya Liberia ambayo imeshuhudia zaidi ya maambukizi elfu kumi na vifo zaidi ya elfu nne tangu ugonjwa wa Ebola kugunduliwa nchini humo.
No comments:
Post a Comment