Operesheni ya jeshi la Urusi nchini Syria inaongeza idadi ya wakimbizi wanaosafiri kwenda Ulaya, Rais wa Baraza la Umoja wa Ulaya, Donald Tusk ameeleza.
Urusi imekuwa ikitekeleza mashambulizi ya anga ikidai kulenga IS.
Lakini wengi wanahofu kuwa nia ya Urusi ni kuendelea kumuweka mshirika wake, Rais wa Syria, Bashar Al Assad madarakani.
Mkutano wa G20 wa viongozi wa dunia ulilenga maswala ya uchumi, lakini mkutano huo wa siku mbili ulitawaliwa na tukio la mashambulizi ya Paris.
No comments:
Post a Comment