Umoja wa Afrika leo unaanza mkutano wa siku mbili utakaofanyika Zambia kukomesha ndoa za utotoni barani.
Mamia ya wasichana wa kike waliokuwa na ndoto za kuenda shule wamejikuta wakilazimika kuwa mama, baada ya kulazimisha kuolewa mapema.
Nyingi ya ndoa hizo za mapema hufanyika vijijini, ambako utamaduni bado unanguvu.
Umoja wa Afrika na mashirika mbalimbali yasiyo ya kiserikali yameunganisha nguvu kushawishi serikali mbalimbali kufanya ndoa za utotoni kama jambo lisilo halali kisheria, kutokana na kukinza haki ya mtoto kupata elimu na pia kumuathiri afya yake.
No comments:
Post a Comment